Urembo Ni Hulka, Sura Ni Sanamu Poem by Winnie Akinyi

Urembo Ni Hulka, Sura Ni Sanamu

Anayenipenda leo, kesho siwezi dhamini.
Naweza kuwa Romeo, nife bilayo imani.
Vitendo kama video, mie siwezi dhamini.
Nisije kawa mumeo, hatima niumie moyoni.
Urembo ni hulka, sura ni saamu.

Mapenzi kama karata, kupata na kupotea.
Ulimbwende siyafuata, ndanimo imeozea.
Hata mwendo kama wa bata, sitamani si'rekea.
Mwiliye sije kunguta, ukahaba kabobea.
Urembo ni hulka, sura ni sanamu.

Wa kupenda ni wengi, wa kuishi ni nadra.
Ndoa hufanya mingi, ila huishi talaka.
Maanani kwa rangi, usitilie kwani ni mafuta.
Siri kama mtungi, ukiyajua utachizika.
Urembo ni hulka, sura ni sanamu.

Chemacho chajiuza, kibaya chajitembeza.
Ujuzi kwake ajuza, sikose kuwauliza.
Usiishipo kwa giza, ukaja kajipumbaza.
Mapenzi ni kuyakuza, sivyo utajiumiza.
Urembo ni hulka, sura ni sanamu.

Urembo Ni Hulka, Sura Ni Sanamu
Wednesday, November 8, 2017
Topic(s) of this poem: beauty,death,lifestyle,love,secrets,trust
POET'S NOTES ABOUT THE POEM
This is a Swahili love poem.
COMMENTS OF THE POEM
Linet 08 November 2017

Nice piece. I enjoyed reading.

1 0 Reply
Winnie Akinyi 09 November 2017

thanks dear i appreciate

0 0
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Close
Error Success